Jinsi ya kupika Half cake
Mahitaji
Unga wa ngano kikombe 1na1/2 (kama robo hivi)
Sukari 1/4 kikombe
Baking powder 1/2 kijiko cha chai
Magadi soda (bicarbonate soda/baking soda) 1 kijiko cha chai
Mafuta 2 vijiko vya chai
Mafuta ya kukaangia
Maji ya uvuguvugu kiasi
Matayarisho
Changanya unga na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande (hakikisha unakuwa mgumu) Baada ya hapo sukuma na ukate shape uipendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio kama mandazi) Baada ya hapo ziweke sehemu yenye joto na uache ziumuke. Zikisha umuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani. Zikisha iva zitoe na uziweke katika kitchen towel ili zichuje mafuta. Ziache zipoe na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
dondoo muhimu:-👇👇👇👇👇
Jinsi ya kupika half keki zilizo pasuka na kuiva vizuri.
1.Hakikisha unatumia vipimo sahihi bila kusahau bicarbonate of soda(baking soda) hiki ndicho kiungo muhimu ktk half cake na baking powder...(hamira SI lazima kuweka kwa half cake za kula tu...labda ziwe za biashara)
2.Unga wako unapokanda uwe mgumu hata kidole kishindwe kupenya kwenye unga
Hauhitaji kuikanda sana kama maandazi ukishashikana tu inatosha.
3.Weka half keki zako kwenye mafuta kabla hayajapata moto.
4.Poza mafuta yako kila baada ya mpiko mmoja.(unaeza kuepua ili yapoe chini...au ukaongeza mafuta ya baridi jikoni )
How to cook half cake
Requirements
Wheat flour 1 and 1/2 cups (about a quarter)
Sugar 1/4 cup
Baking powder 1/2 teaspoon
Magadi soda (bicarbonate soda/baking soda)
1 teaspoon
Oil 2 teaspoons
Frying oil
Relatively lukewarm water
Preparation
Mix the flour and all the ingredients (minus
the cooking oil) then knead it (make sure it's
hard) After that push and cut the shape you
like (make sure you cut thick pieces and not
like mandari) After that put them in a warm
place and let them dry. Bring them to a boil
and fry them in a small fire so that they are
cooked inside. After cooking, take them out
and put them in a kitchen towel to filter the
oil. Let them cool and then they will be
ready to eat.
important extract:-👇👇👇👇👇
How to cook half cakes that are cracked and
cooked well.
1. Make sure you use the correct measurements
without forgetting bicarbonate of soda (baking
soda), this is the most important ingredient
for half cakes and baking powder...
2. When kneading your dough, it should be hard
so that your finger cannot penetrate the dough
You don't need to knead it as much as the buns,
once you stick together it's enough.
3. Put your half cakes in the oil before it
gets hot.
4. Cool your oil after one spoon.
Comments
Post a Comment